Mambo vipi wazeyaaaaa nipo kwenye mishe misheza kuhama so sijatulia lakini msikonde baada ya muda fulani kila kitu kitakwenda sawa...kwa sasa sipo tena TANZANIA DAIMA na SAYARI...nimehamia kwa wajanja wa town kwenye gazeti la CHAMPIONI kama vipi nitawajulisha kila kitu kuhusu job yangu mpya....
John Joseph
Tuesday, December 1, 2009
Saturday, November 21, 2009
RATIBA YA WIKI YA BILICANS
Bilicanas Weekly Program
Wednesdays-
• Ngoma Afrika
• Entrance-5,000 tsh.
• Entertainment- Live Band, Dance Group
Thursdays-
• Ladies Paradise
• Entrance Ladies Free and Gents 5,000 tsh. With 5,000 drink coupon.
• Entertainment- Band + other entertainment.
Fridays-
• Zain Wonders Party
• Entrance 10,000 tsh
• Entertainment-Dancers and Dance Cages, Guest Djs/Competitions- Sexy Street Fashion Show- Extreme Pleasure All Night!!
Saturdays-
• Crazy Saturday Night Live with East Africa
• Entertainment-Live Video Mix- Dance Performance (MJ)-Dance Competitions and Mc Competitions + Dancers and cages. Pure Ecstasy!
• Entrance 10,000 tsh
Sunday-
• Way Back Sundays
• Live Band and Old School Sundays
• Entrance 5,000 tsh
• Entertainment-Live Band, Dj Music.
MWANAMBOKA KUWAONGOZA WENZAKE JUMAPILI HII

Na John Joseph
TAMASHA maalum la watoto linalojulikana kwa jina la Red Ribbon Children's Day linatarajia kufanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kesho kutwa kwa kushirikisha wanamitindo kadhaa maarufu wa hapa nchini.
Katika taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Tanzania Mitindo House (TMH) Khadija Mwanamboka ambao ndio waandaaji wa tamasha hilo, alisema wabunifu hao wameamua kushiriki ili kutoa burudani kwa watoto ili kuwaonyesha jinsi wanavyowajali. Pia alisema watakuwepo wasanii wa muziki wa kiazazi kipya watakaosindikiza shughuli hiyo.
Wanamuziki hao ni Marlaw, Hemed, Profesa Jay, Mo Racka, Matonya, Chid Benz na Quick Rocka ambao watataoa burudani kwa watoto na wengineo watakaofika siku hiyo kushuhudia.
Aidha alitaja wanamitindo wengine watakaokuwepo siku hiyo na kuonyesha ufundi wao wa kucheza muziki ni Mustafa Hassanali, Ally Remtullah, Franko, Zamda George, Farha Sulatan na Asia Idarous atakaecheza ngoma ya kizanzibari itwayo ‘Bomu’.
Pia kutakuwa na mashindano ya kuimba na kucheza na zawadi nyingi zitatolewa kwa watoto. Sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo ni Clouds FM, Channel TEN, Entertainment Masters, Profesa Jay Foundation, Tanzania House of Talent (THT), Mokasi Medical System, Cool Blue na Shear Illusion.
MWISHO
Friday, November 20, 2009
MPOKI WA ZE KOMEDI APATA AJALI NA KUVUNJIKA MKONO

Mpoki, mwigizaji maarufu wa kundi la Ze Original Komedy (kulia) amepata ajali ya gari usiku wa kuamkia jana, na inasemekana amevunjika mkono wake wa kushoto ambapo mfupa umeachia.
Habari kutoka ndani ya kundi hilo zinasema hali yake sio mbaya sana na jana aliruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospitali ya Kairuki iliyoko mikocheni jijini Dar, na ataendelea na matibabu akiwa nyumbani.
Ajali hiyo ilitokea mikocheni wakati gari alilokuwa anaendesha lilipogongana uso kwa uso na Rav4 iliyokuwa inaendeshwa na mwanamama ambaye naye kalazwa hospitali ya TMJ.
Sunday, November 15, 2009
JOHN JOSEPH HARAMBA NA WADAU TUKIJIACHIA
SEVEN NA SALEH ALLY
ELIZABETH WA BIG BROTHER AKIYARUDI MANGOMA
JK AKIWA NA JD NA G. HABASH
RAIS WA FIFA vs RAIS WA NIGERIA
MWENDO WA MAUZO KWA KWENDA MBELE
KOMBE LA BARCLAYS LIKIWA NA WABONGO
HUZUNI UJERUMANI
Thursday, November 12, 2009
ELIZABETH AKIWASILI BONGO
Sunday, November 1, 2009
MB DOG YUPO NJIA PANDA
UNIQ MODOZZ KUPATIKANA BONGO

MMOJA kati ya wadau wa urembo nchini Taji Liundi ambaye anamiliki mtandao wa komputa wa modotz.blogspot.com, ameandaa shindano la kuwapata wanamitindo chipukizi mchakato utakaofanyika hivi karibuni na kujulikana kwa jina la Uniq Modo.
Akielezea mchakato huo alisema hawatozingatia kimo cha washiriki tofauti na dhana iliyopo kuwa mwanamitindo lazima awe mrefu. “Hata kwa wale ambao hawatabahatika kushinda, tutahakikisha inawajali kwa kuwatafutia kazi mbalimbali za uanamitindo kwa wale watakaoonyesha kuwa na nia ya kujiendeleza kwenye fani hiyo.” alisema
Alifafanua kuwa shindano la Uniq Modo ni mwanzo wa safari ndefu ambayo itafungua njia kwa vijana wengi wenye nia na vipaji vya fani hiyo kuweza kujitangaza kitaifa na kimataifa.
MWISHO
Sunday, October 18, 2009
Nameless na Wahuu kufunika malipo ya ‘COSOTA’ ya Kenya
WANAMUZIKI wa Kenya wameanza kuneemeka kwa kupata faida ya kujiandikisha katika Chama cha Haki Miliki nchini humo (MCSK) kutokana na wengi wao kujiandikisha.
Akielezea hali hiyo mwenyekiti wa MCSK, Habel Kifoto alikiri kuwa kuna wanamuziki ambao wameshaanza kupata malipo yao kutokana na kujiandikisha kwenye utaratibu huo.
“Tutazunguka nchi nzima kuweza kutangaza umuhimu wetu na kila mwanamuziki au kikundi cha muziki kitatakiwa kuopata malipo yake kutoka katika kituo cha karibu pasipo kupata usumbufu wowote” alisema
Kwa mujibu wa habari zisizo thibitishwa Nameless na mkewe Wahu ni nyota wanaotarajiwa kupata mauzo makubwa zaidi.
MSHINDI WA BSS 2009!!!
JOHN JOSEPH HARAMBA NILIKUWEMO PIA
ZITTO KABWE NDANI YA DIAMOND JUBELEE
BEATRICE NDANI YA DIAMOND JUBELEE
SHAA JUKWAANI
CASSIAN AKIKAMUA JUKWAANI
UNAMJUA HUYU!!!!!!!
JAMANI WADAU MNAMKUMBUKA RAS INNO AKIWA NA JAKAYA!!!

Ras Inno, akipokea tuzo ya 2001 kutoka kwa Jakaya Kikwete aliyekuwa waziri wa Mambo ya nje enzi hizo ambaye kwa sasa ndiye Presidaa wa Bongo. Katikati ni Hayati Mbamba. Kwa nyuma anayeonekana kwa mbali ni mmoja kati ya waimbaji a kundi la Unique Sister.
Picha kwa hisani ya Ras INNO mwenyewe.. Mzazi endelea kukamia kwa sana tunakuaminia....it me JOHN JOSEPH HARAMBA
Sunday, October 11, 2009
BSS KWENYE INTERVIEW
Sunday, September 27, 2009
JAMANI MODO WETU HUYU, ANAKULA SHAVU STATE
NAME: JIMMY NGANYANGE
SUIT SIZE: 38
HEIGHT:
SHIRT:17
WAIST:34
ISEAM34
SHOE:12
BORN N RAISE: MOROGORO TANZANIA
CURRENT LOCATION: LOS ANGELOS CALIFORNIA
I ACTUALY GOT TWO DEAL WITH OTHER AGENCY CALLED YOUNG AGENCY MODELING I HAVE BEEN WITH THEM FOR ABOUT I JUST GOT INTO FORD NOT LONG AGO.SIMJUI MILLEN BADO MPYA KWENYE AGENCY PLUS FORD NI KUBWA ME NIPO FORD YA WEST COAST SHE MIGHT SOMEWHERE ELSE. BEEN MODELING ON N OFF FOR ABOUT 4YRS. LET ME KNOW IF U NEED MORE INFO BUT I SEND U 5 PHOTOS. GOD BLESS THX
Thursday, September 24, 2009
Fay kumsambaza shemeji
MWANADADA Faidha Omari ‘Sister Fay’ amekamilisha kurekodi video ya wimbo unaojulikana kwa jina la ‘Shemeji’, utakaoanza sambazwa kwenye vyombo vya habari hivi karibuni.
Kwa mujibu wa meneja wa msanii huyo Man Simba alisema mteja wake amepania kurejesha heshima ya jina lake kwenye fani hiyo baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu. “Kutokana na mambo kwenda kwa kasi tunatarajia kuanza kuisambaza video hiyo wiki ijayo” alisema Simba
Fay aliyewahi kuwa mwigizaji wa filamu kabla ya kujitosa kwenye muziki anafannya shughuli zake za kimuziki chini ya studio ya King J Records iliyopo Tabata Jijini.
'Utaipenda’ yawakutanisha Machozi na Joh Makini
‘
HUSSEIN Machozi anayekamata kwenye medani ya muziki kupitia wimbo wa ‘Kwaajili Yako’, ameshirikiana na Joh Makini kutengeneza wimbo wa pili utakaofuatia kutoka kwenye vyombo vya habari, unaojulikana kwa jina la ‘Utaipenda’.
Kwa mujibu wa Meneja wa msanii huyo Sandu Mpanda ‘Kid Bway’ ambaye pia amekuwa akitayarisha nyimbo za Machozi kutoka studio ya Tetemesha Records iliyopo Mwanza alisema video ya wimbo wa ‘Utaipenda’ ipo kwenye hatua za mwisho, ukiwa umetengenezwa na Adam Juma wa kampuni ya Visual Lab.
Wimbo huo nao unapatika kwenye albamu ya ‘Kwa Ajili Yako’. Machozi aliwahi kutamba na nyombo za ‘Kafia Ghetto’, ‘Maji Yakimwagika’ na ‘Full Shangwe’.
Bifu ya Tunda Man na Spark yavunja filamu

KUFUATIA kuibuka kwa majibizano ya maneno ‘bifu’ kati ya wanamuziki Tunda Man na Spark walioimba wimbo wa ‘Nipe Ripoti’, hatma ya filamu yao iliyotokana kwa jina la ‘Nipe Ripoti’ haijulikani.
Filamu hiyo ilikuwa ijulikane kwa jina la ‘Nipe Ripoti’ iliyotokana na hadithi iliyokuwemo ndani ya wimbo huo, ilikuwa ikitengenezwa na kampuni ya video ya Kallage Pictures, ilisimama kutengenezwa kutokana na sababu ambazo hazikuwekwa wazi.
Tunda Man na Spark waliokuwa wahusika wakuu kwa sasa hawaelewani mara baada ya Spark kujitoa kwenye kundi la Tip Top. Wahusika wote hawakuwa tayari kuzungumzia suala hilo isipokuwa Spark aliyesema filamu hiyo haipo tena.
Sunday, September 6, 2009
WANAMITINDO NJE YA NJENGO..PANDE ZA DODOMA
HAPA AY HAPA JAY Z>>>>>
KWANINI SPARK KAJITOA TIP TOP!!!

Hatma ya kundi la Tip Top licha ya kunganisha nguvu na kundi la TMK Family inaonekana kutumba, kutokana na kuendelea kujitoa kwa wasanii katika kundi hilo. Baada ya kujitoa kwa MB Dog, kisha Z Anto na sasa Spark ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo.
Swali linalobaki kichwani ni kwanini Spark amejitoa kwenye kundi hilo licha ya kuwa linaonekana kuwapa mafanikio wasanii wengi.
STOPA NA DJ TASS
Sunday, August 30, 2009
Sunday, August 2, 2009
MAPACHA WA HIP HOP WAJITOSA KWENYE MUVI

Wasanii wawili wa muziki wa Hip Hop nchini wanaojulikana kwa jina la ‘Mapacha’ Levison Kasulwa na James Kasulwa wameamua kujitosa katika uigizaji wa filamu kwa kile walichosema wanataka kujaribu maisha ya upande huo.
Mapacha waliotamba na nyimbo za ‘50 50’, ‘Jipe Moyo’ na ‘Sababu Ya Pesa’ wanatarajia kushiriki katika filamu inayojulikana kwa jina la ‘Sizya’ ambapo wao ndio waigizaji wakuu pamoja na mkongwe wa filamu nchini Lumele Matovolwa maarufu kwa jina la ‘Bigie’.
“Waandaaji wa filamu hiyo kampuni ya Chapakazi waliona tunafaa na wakaamua kutushirikisha katika filamu hiyo lakini haina maana tumeiweka kando iliyotupa umaarufu” alisema Levison
MAYA: BADO NIPO NIPO KWENYE FANI
Maya ni mmoja kati ya waigizaji aliyetamba mwanzoni mwa miaka ya 2000 katika michezo kadhaa ya televisheni iliyokuwa ikionyeshwa na kituo cha ITV ambayo iligizwa na kikundi cha Kaole Sanaa Group, amesema bado anaendeleza fani hiyo licha ya kutoonekana mara kwa mara katika vipindi hivyo.
“Nimeajiriwa kwenye kampuni ya Game 1st Quality inayojihusisha na masuala ya filamu, hivyo akili yangu yote ipo kwenye kuigiza filamu na sio maigizo ya kwenye televisheni.” Alifafanua Maya
Alisema ameamua kujibidiisha kwenye filamu kwakua zinalipa tofauti na maigizo ya kwenye televisheni, pia nia yake ni kujiendeleza kimataifa akidai Game 1st Quality wana malengo mazuri na wasanii wanaofanya nao kazi akimtolea mfano Kanumba kwa kusema kampuni hiyo imemsaidia kuonekana na kufika mbali.
ALLY CHOKI YUPO KENYA

Video za Extra Bongo kurekodiwa Kenya
Kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Ally Choki yupo jijini Nairobi nchini Kenya kwaajili ya kuandaa mazingira ya kurekodia video za nyimbo zao mpya.
Katika ziara hiyo Choki alisema yupo nchini humo kwaajili ya kuongea na kampuni itakayotumika kurekodi video hizo japo alisema ni mapema mno kutaja jina la kampuni hiyo na kuahidi ataweka wazi mara atakaporejea nchini.
Albamu ya Extra Bongo inayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni ikijulikana kwa jina la ‘Mjini Mipango’ ambao ni jina la moja ya wimbo unaopatikana ndani ya albamu hiyo ikiwa ni utunzi wa Choki mwenyewe.
NIMECHILL NA TWINS!!!
Sunday, July 26, 2009
DROGBA AHAMIA KWENYE KIKAPU
Subscribe to:
Posts (Atom)