
Video za Extra Bongo kurekodiwa Kenya
Kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Ally Choki yupo jijini Nairobi nchini Kenya kwaajili ya kuandaa mazingira ya kurekodia video za nyimbo zao mpya.
Katika ziara hiyo Choki alisema yupo nchini humo kwaajili ya kuongea na kampuni itakayotumika kurekodi video hizo japo alisema ni mapema mno kutaja jina la kampuni hiyo na kuahidi ataweka wazi mara atakaporejea nchini.
Albamu ya Extra Bongo inayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni ikijulikana kwa jina la ‘Mjini Mipango’ ambao ni jina la moja ya wimbo unaopatikana ndani ya albamu hiyo ikiwa ni utunzi wa Choki mwenyewe.
No comments:
Post a Comment