
Wasanii wawili wa muziki wa Hip Hop nchini wanaojulikana kwa jina la ‘Mapacha’ Levison Kasulwa na James Kasulwa wameamua kujitosa katika uigizaji wa filamu kwa kile walichosema wanataka kujaribu maisha ya upande huo.
Mapacha waliotamba na nyimbo za ‘50 50’, ‘Jipe Moyo’ na ‘Sababu Ya Pesa’ wanatarajia kushiriki katika filamu inayojulikana kwa jina la ‘Sizya’ ambapo wao ndio waigizaji wakuu pamoja na mkongwe wa filamu nchini Lumele Matovolwa maarufu kwa jina la ‘Bigie’.
“Waandaaji wa filamu hiyo kampuni ya Chapakazi waliona tunafaa na wakaamua kutushirikisha katika filamu hiyo lakini haina maana tumeiweka kando iliyotupa umaarufu” alisema Levison
No comments:
Post a Comment