Sunday, August 2, 2009

MAYA: BADO NIPO NIPO KWENYE FANI




Maya ni mmoja kati ya waigizaji aliyetamba mwanzoni mwa miaka ya 2000 katika michezo kadhaa ya televisheni iliyokuwa ikionyeshwa na kituo cha ITV ambayo iligizwa na kikundi cha Kaole Sanaa Group, amesema bado anaendeleza fani hiyo licha ya kutoonekana mara kwa mara katika vipindi hivyo.

“Nimeajiriwa kwenye kampuni ya Game 1st Quality inayojihusisha na masuala ya filamu, hivyo akili yangu yote ipo kwenye kuigiza filamu na sio maigizo ya kwenye televisheni.” Alifafanua Maya

Alisema ameamua kujibidiisha kwenye filamu kwakua zinalipa tofauti na maigizo ya kwenye televisheni, pia nia yake ni kujiendeleza kimataifa akidai Game 1st Quality wana malengo mazuri na wasanii wanaofanya nao kazi akimtolea mfano Kanumba kwa kusema kampuni hiyo imemsaidia kuonekana na kufika mbali.

No comments: