Kuna washkaji watatu walikuwa wamechill kwenye chumba flani hivi wanapuliza kitu cha A-City aka Majani, basi bwana mjani ukiwa umekolea kibiriti walichokuwa wakikitumia kikawa kimeisha na still walikuwa wanakihitaji kukitumia ikabidi wamtume mwenzao mmoja kwenda kutafuta kibiriti, mchizi hakupinga ikabidi atoke nje kwenda kuatafuta kibiriti.
Mchizi alipofika nje akazunguka nje ya nyumba hilehile waliyokuwemo kisha akarudi kwa wale wale wana wake alipowakuta akaanza kusemesha huku akiwa anayumba yumba “Oya eehe machizi naombeni kiberiti kama kuna mtu anacho kati yenu?”
Wale wawili waliokuwa wamekaa wakamjibu “Kuna mwenetu mmoja ameenda kuazima hapo jirani kama vipi njoo tumsubiri atarudi muda sio mrefu”.
Wednesday, November 5, 2008
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment