Tuesday, September 14, 2010

NIPO BIZE WANAAAAAAAA

Wazeyaaa nipo bize mbaya ndiyo maana nakuwa lesi nakosa hata time ya ku up date blog yangu ila msikonde wanawane maana najua Blog imekuwa kama fasheni pande hizi kwa sasa kila mtu anayo duuu mpaka naona kama vipi nifungue mambo ya WEBSITE..............

EMINEM AKAMUA MBAYAAA



Jamaa Eminem na kiburudisho wa zamani wa Chriss Brown, hapa namzungumzia Rihanna wamekamua mbaya juzi kati kwenye tuzo za MTV

Tuesday, March 23, 2010

SIMBA, MABINGWA WA TANZANIA



KIKOSI CHA SIMBA AMBACHO KIMETWA UBINGWA WA TANZANIA BARA MWAKA 2010.

MZAMBIA AKIANGALIA MASHABIKI


KOCHA MZAMBIA PATRICK PHIRI AKIWA NA MENEJA WA SIMBA INNOCENT NJOVU WAKILONGA MAMBO MAWILI MATATU...PHIRI AMEKUWA ANI KOCHA MWENYE MAFANIKIO KATIKA KLABU YA SIMBA KILA ANAPOTUA TANZANIA KUKIKOA KIKOSI HICHO






imeandikwa na John Joseph

KIDEDEAAA


MASHABIKI WA MSIMBAZI WAKISHANGILIA UBINGWA MARA BAADA YA KUIFUNGA AZAM NA KUWAWEZESHA KUTANGAZA UBINGWA HATA KABLA YA KUMALIZIKA KWA LIGI WAKIWA NA MECHI MBILI MKONONI

Sunday, March 14, 2010

TUKISHUUDIA MTANGANGE



Mtu mzima, John Joseph Haramba nikiwa na members wenzangu wa Global katika tukishuhudia mitanange ya NSSF. Mimi ni wa kwanza kulia nikifuatiwa na Samirah Phillip, Theodora Mbwana na Leah Kweka

KIKOSI CHA MAUAJI



Kikosi cha Global kikiwa kabla ya kuanza mtanange kwenye mchezo mmoja katika ligi ya NSSF mwaka 2010.

ORIGINAL AU MCHINA??


Dada zetu inabidi tuwe makini, hivi kweli haya ni maumbo yake kweli auuuu

Tuesday, December 1, 2009

NIMEHAMIA GAZETI LA CHAMPIONI KWA SASA

Mambo vipi wazeyaaaaa nipo kwenye mishe misheza kuhama so sijatulia lakini msikonde baada ya muda fulani kila kitu kitakwenda sawa...kwa sasa sipo tena TANZANIA DAIMA na SAYARI...nimehamia kwa wajanja wa town kwenye gazeti la CHAMPIONI kama vipi nitawajulisha kila kitu kuhusu job yangu mpya....
John Joseph

Saturday, November 21, 2009

RATIBA YA WIKI YA BILICANS


Bilicanas Weekly Program

Wednesdays-
• Ngoma Afrika
• Entrance-5,000 tsh.
• Entertainment- Live Band, Dance Group

Thursdays-
• Ladies Paradise
• Entrance Ladies Free and Gents 5,000 tsh. With 5,000 drink coupon.
• Entertainment- Band + other entertainment.

Fridays-
• Zain Wonders Party
• Entrance 10,000 tsh
• Entertainment-Dancers and Dance Cages, Guest Djs/Competitions- Sexy Street Fashion Show- Extreme Pleasure All Night!!

Saturdays-
• Crazy Saturday Night Live with East Africa
• Entertainment-Live Video Mix- Dance Performance (MJ)-Dance Competitions and Mc Competitions + Dancers and cages. Pure Ecstasy!
• Entrance 10,000 tsh

Sunday-
• Way Back Sundays
• Live Band and Old School Sundays
• Entrance 5,000 tsh
• Entertainment-Live Band, Dj Music.

HAINA KUSHANGAA



Huyu jamaa kwao ndiyo HANDSOME

HII NDIO BONGOOOO!!!



Haina kushangaa, gari inaenda huku mlango unabaki nyuma....

MWANAMBOKA KUWAONGOZA WENZAKE JUMAPILI HII



Na John Joseph

TAMASHA maalum la watoto linalojulikana kwa jina la Red Ribbon Children's Day linatarajia kufanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kesho kutwa kwa kushirikisha wanamitindo kadhaa maarufu wa hapa nchini.

Katika taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Tanzania Mitindo House (TMH) Khadija Mwanamboka ambao ndio waandaaji wa tamasha hilo, alisema wabunifu hao wameamua kushiriki ili kutoa burudani kwa watoto ili kuwaonyesha jinsi wanavyowajali. Pia alisema watakuwepo wasanii wa muziki wa kiazazi kipya watakaosindikiza shughuli hiyo.

Wanamuziki hao ni Marlaw, Hemed, Profesa Jay, Mo Racka, Matonya, Chid Benz na Quick Rocka ambao watataoa burudani kwa watoto na wengineo watakaofika siku hiyo kushuhudia.

Aidha alitaja wanamitindo wengine watakaokuwepo siku hiyo na kuonyesha ufundi wao wa kucheza muziki ni Mustafa Hassanali, Ally Remtullah, Franko, Zamda George, Farha Sulatan na Asia Idarous atakaecheza ngoma ya kizanzibari itwayo ‘Bomu’.

Pia kutakuwa na mashindano ya kuimba na kucheza na zawadi nyingi zitatolewa kwa watoto. Sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo ni Clouds FM, Channel TEN, Entertainment Masters, Profesa Jay Foundation, Tanzania House of Talent (THT), Mokasi Medical System, Cool Blue na Shear Illusion.


MWISHO

Friday, November 20, 2009

MPOKI WA ZE KOMEDI APATA AJALI NA KUVUNJIKA MKONO



Mpoki, mwigizaji maarufu wa kundi la Ze Original Komedy (kulia) amepata ajali ya gari usiku wa kuamkia jana, na inasemekana amevunjika mkono wake wa kushoto ambapo mfupa umeachia.
Habari kutoka ndani ya kundi hilo zinasema hali yake sio mbaya sana na jana aliruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospitali ya Kairuki iliyoko mikocheni jijini Dar, na ataendelea na matibabu akiwa nyumbani.
Ajali hiyo ilitokea mikocheni wakati gari alilokuwa anaendesha lilipogongana uso kwa uso na Rav4 iliyokuwa inaendeshwa na mwanamama ambaye naye kalazwa hospitali ya TMJ.

Sunday, November 15, 2009

JOHN JOSEPH HARAMBA NA WADAU TUKIJIACHIA



Hapa mtu mzima nilikuwa na washkaji na wafanyakazi wenzangu tukijiachia, ilikuwa ni furaha tupu ndani ya BILICANAS

SEVEN NA SALEH ALLY



SEVEN AKIYARUDI NA SALEH ALLY KWENYE WELCOME PARTY YA ELIZABETH WA BIG BROTHER KWENYE UKUMBI WA BILICANAS

HATA MIMI NIMO !!!



Hata mimi mdau wenu JOHN JOSEPH nilikuwepo na dada Lucy Kiwere...mnamkumbuka??

ELIZA IF U DO ME I DO U



MAMBO YALIKUWA SIO MCHEZO!! HAPA ELIZABETH ALIKUWA AKICHEZA HUKU AMEZYNGUKWA NA WADAU KIBAO...

ELIZABETH WA BIG BROTHER AKIYARUDI MANGOMA



\Mwakilishi wa TANZANIA katika shindano la Big Brother, Elizabeth Gupta akiwa anayarudi mangoma katika sherehe maalum ya kumkaribisha iliyofanyika kwenye ukumbiwa BILICANAS mwishoni mwa wiki hii... mambo yalikuwa sio mchezo

NAOMI NDANI YA BONGO.



Mwanamitindo wa kimataifa kutoka Marekani Naomi Campbel akiwa ndani ya Bongo hivi karibuni.

JK AKIWA NA JD NA G. HABASH



Judith Wabura aka Lady Jay Dee akiwa pamoja na Jakaya Kikwete pamoja na mumewe Gadner G. Habash wakati wa hafla ya MO Ibrahimu iliyofanyika Dar es salaam mwishoni mwa wiki huu

RAIS WA FIFA vs RAIS WA NIGERIA



Rais wa FIFA, Joseph Sepp Blatter (kushoto) akikabidhi medali ya FIFA KWA Rais wa Nigeria , Umaru Yar'Adua mnamo Novemba 15, katika mji wa Abuja.

MWENDO WA MAUZO KWA KWENDA MBELE



Mshkaji wangu anayepiga mzigo katika kituo cha MLIMANI TV, akiwa kwenye pozi na kombe la Ligi Kuu ya England.

KOMBE LA BARCLAYS LIKIWA NA WABONGO



Kombe la ligi kuu ya soka ya England lilipotua Bongo, fans kibao walijitokeza kupokea Kama wanavyoonekana baadhi ya wadau wakipozi kwaajili ya picha.

HUZUNI UJERUMANI



Wachezaji wa soka wa Ujerumani wakibeba jeneza lenye mwili wa kiwa wa nchi hiyo aliyejiua wakati wa kuuaga mwili wake.

Thursday, November 12, 2009

ELIZABETH GUPTA AKIINGIA BONGO



Elizabeth alipokuwa kiikanyaga ardhi ya Bongo mara baada ya kuwasili Jumatano ya wiki hii.

ELIZABETH AKIWASILI BONGO



Mshiriki wa Tanzania aliyekuwepo kwenye jumba la Big Brother akiwasili kutoka Afrika Kusini alipokuwa akishiriki baada ya kutolewa kwenye kinyang'anyiro hicho wiki iliyopita. Hapa likuwa amemkumbatia mtoto wa mmoja kati ya ndugu zake wealiofika kumpokea uwanja wa ndege

Sunday, November 1, 2009

MB DOG YUPO NJIA PANDA



KUMEKUWA na taarifa kuwa MB Dog aliyejitoa katika kundi la Tip Top CONNECTION yupo njia panda kuhusu kurejea kundini au la kutokana na kuyumba katika kujisimamia kazi zake. Tangu alipotoka kundini mwaka jana hajatoa albamu nyingine tangu ile ya kwanza ya ‘Ratifa’ aliyokuwa chini ya Tip Top.

UNIQ MODOZZ KUPATIKANA BONGO



MMOJA kati ya wadau wa urembo nchini Taji Liundi ambaye anamiliki mtandao wa komputa wa modotz.blogspot.com, ameandaa shindano la kuwapata wanamitindo chipukizi mchakato utakaofanyika hivi karibuni na kujulikana kwa jina la Uniq Modo.

Akielezea mchakato huo alisema hawatozingatia kimo cha washiriki tofauti na dhana iliyopo kuwa mwanamitindo lazima awe mrefu. “Hata kwa wale ambao hawatabahatika kushinda, tutahakikisha inawajali kwa kuwatafutia kazi mbalimbali za uanamitindo kwa wale watakaoonyesha kuwa na nia ya kujiendeleza kwenye fani hiyo.” alisema

Alifafanua kuwa shindano la Uniq Modo ni mwanzo wa safari ndefu ambayo itafungua njia kwa vijana wengi wenye nia na vipaji vya fani hiyo kuweza kujitangaza kitaifa na kimataifa.



MWISHO

Sunday, October 18, 2009

Nameless na Wahuu kufunika malipo ya ‘COSOTA’ ya Kenya



WANAMUZIKI wa Kenya wameanza kuneemeka kwa kupata faida ya kujiandikisha katika Chama cha Haki Miliki nchini humo (MCSK) kutokana na wengi wao kujiandikisha.

Akielezea hali hiyo mwenyekiti wa MCSK, Habel Kifoto alikiri kuwa kuna wanamuziki ambao wameshaanza kupata malipo yao kutokana na kujiandikisha kwenye utaratibu huo.

“Tutazunguka nchi nzima kuweza kutangaza umuhimu wetu na kila mwanamuziki au kikundi cha muziki kitatakiwa kuopata malipo yake kutoka katika kituo cha karibu pasipo kupata usumbufu wowote” alisema

Kwa mujibu wa habari zisizo thibitishwa Nameless na mkewe Wahu ni nyota wanaotarajiwa kupata mauzo makubwa zaidi.

MSHINDI WA BSS 2009!!!



Mshindi wa BSS, Cassian akipungia mashabiki mkono mara baada ya kutangazwa kutwaa kitita cha Shilingi Milioni 25 za kibongo, baada ya kukamua kisawasawa kwenye shoo hiyo, pembeni yake ni Mada Rita aliyemkabidhi mzigo huo.

JOHN JOSEPH HARAMBA NILIKUWEMO PIA



Mtu mzima na mimi nilikuwepo kususza macho nikiwa nimetinga t-shirt ya washkaji zangu 'WABISHI WA TAOWN' ila wananilipa mwana wanee oooh usifikiri navaa kuuza nyago tu.....pembeni yangu kulia na kushoto ni afanyakazi wenzangu.

ZITTO KABWE NDANI YA DIAMOND JUBELEE



Mizuka ilimpanda Mbunge wa Kigoma, Mh Zitto Kabwe katika ukumbi wa Diamond Jubelee na akaamua kuinuka kushangilia kama anavyoonekana, mambo yalikuwa sio mchezo ndani ya ukumbi huo.

BEATRICE NDANI YA DIAMOND JUBELEE



Mshiriki aliyeshina nafasi ya 5, Beatrice William akikamua jukwaani wimbo wa 'Chambua Kama Karanga' ndani ya Diamond Jubelee......

SHAA JUKWAANI



Mwanamuziki Sara Kaisi aka SHAA akiimba siku ya onyesho la BSS KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBELEE. Wanaoonekana kwa pembeni yake na nyuma ni dansers wake aliokuwa nao kutoka Tanzania House of Talent (THT)

CASSIAN AKIKAMUA JUKWAANI



Mshindin wa BSS, Paschal Casssian kutoka Mwanza akikamua jukwaani siku ya Shindano hilo katika ukumbi wa Diamond Jubelee

UNAMJUA HUYU!!!!!!!



Hivi ndivyo alivyokuwa miaka ya 1970, unamjua ni nani huyuuuuuuuu!!!!!

Anaitwa Ras Inno. Kwa ni mwanamuziki mkongwe wa Reggae wa hapa nchini ambaye kwa sasa licha ya kuendelea na kazi ya muziki pia ni mwandishi wa makala na kolam mbali mbali katika magazeti ya TANZANIA DAIMA na SAYARI.

RAS INNO, HIVI SASA



Ras Inno akiwa katika pozi katika picha iliyopigwa hivi karibuni.

RAS INNO JUKWAANI



Ras Inno akiimba jukwaani siku kumuezi Bob Marley mwaka 2003

RAS INNO NDANI YA MAWINGU



Ras Inno akiwa studio pande za Mawingu akifanya mambo.....