Thursday, January 29, 2009

PAMOJA SANA

NIMEWASOMA WATU WANGU WOTE NA NINASHUKURU KWA MAONI YENU..ENDELEENI KUNIMUVUZISHIA KUPITIA haramba29@yahoo.co.uk

SNOOP PAMOJA NA WIZZY


Lil Wayne and Snoop Dogg wanatarajia kutoka na documentary mpya itakayojulikana kwa jina la “Crips and Bloods" kaa tayari kujua zaidi kuhusu inshu hiyo mambo yakiwa tayari kupitia hapa hapa MUZIKI MNENE.

Monday, January 26, 2009

KANYE AJIVUNIA OBAMA



Kanye West amesema anajivunia kuwa mmoja kati ya wasanii walitumbuiza siku ya kuapishwa kwa Rais wa kwanza mweusi wa USA, Kanye amenukuliwa akisema "Natamani marehemu Mama angekuwepo na kuona tukio hili"

YOUNG JEEZY FACE 2 FACE NA MBAYA WAKE




Young Jeezy amekubali mwaliko wa Bil O’Reilly kuweza kutokea kwenye show yake japo mtangzaji huyo aliwaponda Jeezy na Jay Z walipokuwa wakipafom wimbo wa “My President,” ambapo yeye aliwaita kuwa “a rant that offended people” na kusema kuwa hata Obama yawezekan hakufurahishwa na ujumbe wa wimbo huo. Lkini kwa kuonyesha kuwa Young yupo strong kwa kile alichokuwa akikiimba watu hao watakuwa katika show moja wakichati

AKON ADANGANYA UMRI WAKE



Katika kudhihirisha ule msemo wa "Age ain't nothing but a number" Msanii Akon alitoa kali baada ya kudai kuwa yeye hua hafatilii maswala ya miaka yake na hapendi kujua umri wake kwa sasa na sababu kuwa hapendi kujiona akizeeka wakati ndio kwaaza anaanza kupata mafanikio

Katika cheti chake cha kuzaliwa kinaonyesha kuwa Akon anamiaka 31 lakini yeye anasema anajiona ni kijana wa miaka 21 na bado ataendelea kujiona kijana wa miaka hiyo (21) kwa miaka 10 ijayo.

BAB LEE KWENYE GAME TENA



Baada ya kimya cha muda flani mshkaji kutoka crew ya SHAROBARO Bab Lee anatarajia kurejea upya kwenye game akiwa na nguvu full 100% maujuzi, nilipokutana na Baba lee mitaa flani ya Posta kwenye mjengo flani amenidokeza kuwa kwa kuanzia amesha achia kitu kinachojulikan kwa jina la "Chagua Mmoja" ambayo video yake imeanza kuonekana wiki chache zilizopita.

Haina noma mwana mimi pamoja na watu wangu wa MUZIKIMNENE tunakusubiri kwa hamu na tunakwambia WELCOME BACK

Tuesday, January 20, 2009

NYOMI KUMCHEKI OBAMA

OBAMA



RAIS WA USA BARACK OBAMA AKIWA NA KWENYE POZI LA FURAHA MARA BAADA YA KUAPISHWA KUWA RAIS WA 44 WA MAREKANI

BOW WOW & ASHANTI



Bow Wow akiwa katika pozi na shemeji yake Ashanti, Ashanti ni girlfriend wa Nelly ambapo Nelly amekuwa akilalamika nia yake ni kufunga ndoa na kimwana huyo lakini mamayake na Ashanti ndio imekuwa kikwazo kikubwa kutokana na kumwabia binti yake asubiri.

Saturday, January 10, 2009

HII NI FERRY YA DAR SIO MTONI

CHINGA BOY AKIKOMAA NA BIZINESI

HIVI LIKIZO TYME SI IMEISHA AU ???



Hii ilikuwa Jumamosi ya tarehe 10 January 2009 maeneo ya Njia Pnada Ya Kigogo.

NEW BILLLICANAS



Ukumbi wa Billicana katika mwonekano mpya kwa nje, hii ni baada ya kufunguliwa mwanzoni mwa mwezi huu wa kwanza tangu ilipofungwa mwishoni mwa mwaka jana kwaajili ya matengenezo zaidi.

Monday, January 5, 2009

BIASHARA IMEDODA NINI ???



Hili ni moja kati ya bango lililotupu katika makutano ya barabara ya Nyerere na Kawawa.

KIJANA MJASIRIAMALI