Sunday, September 27, 2009

HAPA AKIWA KATIKA POZI TOFAUTI

JAMANI MODO WETU HUYU, ANAKULA SHAVU STATE



NAME: JIMMY NGANYANGE
SUIT SIZE: 38
HEIGHT:
SHIRT:17
WAIST:34
ISEAM34
SHOE:12
BORN N RAISE: MOROGORO TANZANIA
CURRENT LOCATION: LOS ANGELOS CALIFORNIA

I ACTUALY GOT TWO DEAL WITH OTHER AGENCY CALLED YOUNG AGENCY MODELING I HAVE BEEN WITH THEM FOR ABOUT I JUST GOT INTO FORD NOT LONG AGO.SIMJUI MILLEN BADO MPYA KWENYE AGENCY PLUS FORD NI KUBWA ME NIPO FORD YA WEST COAST SHE MIGHT SOMEWHERE ELSE. BEEN MODELING ON N OFF FOR ABOUT 4YRS. LET ME KNOW IF U NEED MORE INFO BUT I SEND U 5 PHOTOS. GOD BLESS THX

Thursday, September 24, 2009

Fay kumsambaza shemeji



MWANADADA Faidha Omari ‘Sister Fay’ amekamilisha kurekodi video ya wimbo unaojulikana kwa jina la ‘Shemeji’, utakaoanza sambazwa kwenye vyombo vya habari hivi karibuni.

Kwa mujibu wa meneja wa msanii huyo Man Simba alisema mteja wake amepania kurejesha heshima ya jina lake kwenye fani hiyo baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu. “Kutokana na mambo kwenda kwa kasi tunatarajia kuanza kuisambaza video hiyo wiki ijayo” alisema Simba

Fay aliyewahi kuwa mwigizaji wa filamu kabla ya kujitosa kwenye muziki anafannya shughuli zake za kimuziki chini ya studio ya King J Records iliyopo Tabata Jijini.

'Utaipenda’ yawakutanisha Machozi na Joh Makini




HUSSEIN Machozi anayekamata kwenye medani ya muziki kupitia wimbo wa ‘Kwaajili Yako’, ameshirikiana na Joh Makini kutengeneza wimbo wa pili utakaofuatia kutoka kwenye vyombo vya habari, unaojulikana kwa jina la ‘Utaipenda’.

Kwa mujibu wa Meneja wa msanii huyo Sandu Mpanda ‘Kid Bway’ ambaye pia amekuwa akitayarisha nyimbo za Machozi kutoka studio ya Tetemesha Records iliyopo Mwanza alisema video ya wimbo wa ‘Utaipenda’ ipo kwenye hatua za mwisho, ukiwa umetengenezwa na Adam Juma wa kampuni ya Visual Lab.

Wimbo huo nao unapatika kwenye albamu ya ‘Kwa Ajili Yako’. Machozi aliwahi kutamba na nyombo za ‘Kafia Ghetto’, ‘Maji Yakimwagika’ na ‘Full Shangwe’.

Bifu ya Tunda Man na Spark yavunja filamu



KUFUATIA kuibuka kwa majibizano ya maneno ‘bifu’ kati ya wanamuziki Tunda Man na Spark walioimba wimbo wa ‘Nipe Ripoti’, hatma ya filamu yao iliyotokana kwa jina la ‘Nipe Ripoti’ haijulikani.

Filamu hiyo ilikuwa ijulikane kwa jina la ‘Nipe Ripoti’ iliyotokana na hadithi iliyokuwemo ndani ya wimbo huo, ilikuwa ikitengenezwa na kampuni ya video ya Kallage Pictures, ilisimama kutengenezwa kutokana na sababu ambazo hazikuwekwa wazi.

Tunda Man na Spark waliokuwa wahusika wakuu kwa sasa hawaelewani mara baada ya Spark kujitoa kwenye kundi la Tip Top. Wahusika wote hawakuwa tayari kuzungumzia suala hilo isipokuwa Spark aliyesema filamu hiyo haipo tena.

Sunday, September 6, 2009

WANAMITINDO NJE YA NJENGO..PANDE ZA DODOMA



Wanamitindo na wabunufu wa mavazimaarufu wa hapa nchini wakiwa kwenye picha ya pamoja nje ya mjengo wa Bunge katika mji wa Dodoma, wabunifu hao walienda kwaajili ya kutembea na shughuli nyinginezo

HAPA AY HAPA JAY Z>>>>>



Mzee wa Biashara, AY akilonga na waandishi wa habari wakati wa kuelezea juu ya safari yao ya kwenye tuzo za MTV (MAMA) zitzkzofanyika Kenya. AY yupo kwenye kipengere kimoja na JAY Z.

Kipengere cha AY ni
Best Hip Hop
M.I. (Nigeria)
A.Y. (Tanzania)
Zulu Boy (South Africa)
Jay-Z (USA)
Kanye West (USA)

KWANINI SPARK KAJITOA TIP TOP!!!



Hatma ya kundi la Tip Top licha ya kunganisha nguvu na kundi la TMK Family inaonekana kutumba, kutokana na kuendelea kujitoa kwa wasanii katika kundi hilo. Baada ya kujitoa kwa MB Dog, kisha Z Anto na sasa Spark ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo.
Swali linalobaki kichwani ni kwanini Spark amejitoa kwenye kundi hilo licha ya kuwa linaonekana kuwapa mafanikio wasanii wengi.

STOPA NA DJ TASS



Msanii wa Bongo Flava, Stopa akiwa ameweka pozi kwaajili ya picha pamoja na DJ Tass wa Radio Magic FM ya Jijini. Stopa ni kati ya wasanii watakao toa shoo ya nguvu kwenye ukumbi wa Dar West uliopo Tabata siku ya Idd Mosi.

Wasanii wegine ni Fid Q, Z Anto, Pingu na wengineo kibao