Sunday, October 18, 2009

Nameless na Wahuu kufunika malipo ya ‘COSOTA’ ya Kenya



WANAMUZIKI wa Kenya wameanza kuneemeka kwa kupata faida ya kujiandikisha katika Chama cha Haki Miliki nchini humo (MCSK) kutokana na wengi wao kujiandikisha.

Akielezea hali hiyo mwenyekiti wa MCSK, Habel Kifoto alikiri kuwa kuna wanamuziki ambao wameshaanza kupata malipo yao kutokana na kujiandikisha kwenye utaratibu huo.

“Tutazunguka nchi nzima kuweza kutangaza umuhimu wetu na kila mwanamuziki au kikundi cha muziki kitatakiwa kuopata malipo yake kutoka katika kituo cha karibu pasipo kupata usumbufu wowote” alisema

Kwa mujibu wa habari zisizo thibitishwa Nameless na mkewe Wahu ni nyota wanaotarajiwa kupata mauzo makubwa zaidi.

MSHINDI WA BSS 2009!!!



Mshindi wa BSS, Cassian akipungia mashabiki mkono mara baada ya kutangazwa kutwaa kitita cha Shilingi Milioni 25 za kibongo, baada ya kukamua kisawasawa kwenye shoo hiyo, pembeni yake ni Mada Rita aliyemkabidhi mzigo huo.

JOHN JOSEPH HARAMBA NILIKUWEMO PIA



Mtu mzima na mimi nilikuwepo kususza macho nikiwa nimetinga t-shirt ya washkaji zangu 'WABISHI WA TAOWN' ila wananilipa mwana wanee oooh usifikiri navaa kuuza nyago tu.....pembeni yangu kulia na kushoto ni afanyakazi wenzangu.

ZITTO KABWE NDANI YA DIAMOND JUBELEE



Mizuka ilimpanda Mbunge wa Kigoma, Mh Zitto Kabwe katika ukumbi wa Diamond Jubelee na akaamua kuinuka kushangilia kama anavyoonekana, mambo yalikuwa sio mchezo ndani ya ukumbi huo.

BEATRICE NDANI YA DIAMOND JUBELEE



Mshiriki aliyeshina nafasi ya 5, Beatrice William akikamua jukwaani wimbo wa 'Chambua Kama Karanga' ndani ya Diamond Jubelee......

SHAA JUKWAANI



Mwanamuziki Sara Kaisi aka SHAA akiimba siku ya onyesho la BSS KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBELEE. Wanaoonekana kwa pembeni yake na nyuma ni dansers wake aliokuwa nao kutoka Tanzania House of Talent (THT)

CASSIAN AKIKAMUA JUKWAANI



Mshindin wa BSS, Paschal Casssian kutoka Mwanza akikamua jukwaani siku ya Shindano hilo katika ukumbi wa Diamond Jubelee

UNAMJUA HUYU!!!!!!!



Hivi ndivyo alivyokuwa miaka ya 1970, unamjua ni nani huyuuuuuuuu!!!!!

Anaitwa Ras Inno. Kwa ni mwanamuziki mkongwe wa Reggae wa hapa nchini ambaye kwa sasa licha ya kuendelea na kazi ya muziki pia ni mwandishi wa makala na kolam mbali mbali katika magazeti ya TANZANIA DAIMA na SAYARI.

RAS INNO, HIVI SASA



Ras Inno akiwa katika pozi katika picha iliyopigwa hivi karibuni.

RAS INNO JUKWAANI



Ras Inno akiimba jukwaani siku kumuezi Bob Marley mwaka 2003

RAS INNO NDANI YA MAWINGU



Ras Inno akiwa studio pande za Mawingu akifanya mambo.....

JAMANI WADAU MNAMKUMBUKA RAS INNO AKIWA NA JAKAYA!!!


Ras Inno, akipokea tuzo ya 2001 kutoka kwa Jakaya Kikwete aliyekuwa waziri wa Mambo ya nje enzi hizo ambaye kwa sasa ndiye Presidaa wa Bongo. Katikati ni Hayati Mbamba. Kwa nyuma anayeonekana kwa mbali ni mmoja kati ya waimbaji a kundi la Unique Sister.

Picha kwa hisani ya Ras INNO mwenyewe.. Mzazi endelea kukamia kwa sana tunakuaminia....it me JOHN JOSEPH HARAMBA

Sunday, October 11, 2009

BSS KWENYE INTERVIEW



Mmoja kati ya washiriki wa BSS, Peter kiwa kwenye interview na mtangzaji mkongwe Godwin Gondwe zamani alijulikana kwa jina la Daouble G.