Sunday, July 26, 2009

DROGBA AHAMIA KWENYE KIKAPU




LaMarcus Aldridge (katikati) nyota wa mchezo wa kikapu wa timu ya Portland Trailblazers, akipozi kwa picha na wachezaji wa Chelsea FC, Didier Drogba (kulia) na Petr Cech mara baada ya kubadilishana jezi, juzi katika uwanja wa Cowboys jijini Texas kutakapofanyika mashindano ya nyota wa NBA.

Monday, July 13, 2009

MBONA UNAGOMA KULIPAA!!!



Dada huyu alikuwa anazinguana na dereva wa tax hii aliyekuwa amegoma kulipa hela ya kupaki gari yake. Halafu chaajabu ndani alikuwa anawateja wazungu....wabongo bwana

Sunday, July 12, 2009

MBIO ZA SKUNA!!!!


Umeipata huyo, kina dada hawa walikimbia umbali wa mita 100 wakiwa wamevaa viatu vyenye urefu wa sentimeta 7 na upana wa sentimeta 1.5

Friday, July 10, 2009

NASHUKURU MDAU WANGU KWA MAONI YAKO

Nashukuru, kuna mdau mmoja amabye hakupenda kujitambulisha kwa jina leo hii asubuhi alinipigia simu na tukaanza kujadiri kuhusu moja kati ya makala yangu ya kwenye GAZETI LA TANZANIA DAIMA niliyokuwa nazungumzia muziki, kwakweli tuliongea kwa kirefu sana na ka mujibu wa maongezi ya huyo mtu naonekana kweli ni mfuatiliaji wa muziki.

Nashukuru mhwshimwa kama utasoma haya maneno yangu, na ninaomba endelea kufuatilia mtandao wangu nakazi zangu na kama kuna chochote unachohisi nimefanya ndivyo sivyo au ungependa kunipongeza, cheki nami kupitia 0713 393542 au kwa email haramba29@yahoo.co.uk

ni wako JOHN JOSEPH HARAMBA wa muzikimnene.blogspot.com

Thursday, July 9, 2009

CHILLAH ANYOA PARA



Msanii wa muziki kipya Abubakar Shabani Katwira aka Q-CHILAH AMENYOA NYWERE ZAKE ALIZODUMU NAZO KWA KIAMA 10. NA KWAMUJIBU WA MTANDAO WA DJCHOKA. NI KUWA KWA SASA Q-CHILLA ANATARAJIA KUCHORA TATOO KICHWANI KWAKE.

Tuesday, July 7, 2009

Chameleone KUANZISHA TAASISI YA KULEA WATOTO




JOSE Mayanja maarufu kwa jina la Jose Chameleone mwanamuziki maarufu wa Uganda anatarajia kuanzisha taasasi itakayo jihusisha na malezi ya watoto.
Taarifa kutoka vyanzo vya habari nchini humo zimesema Chamileone ameonyesha kuwa na nia hiyo ikiwa ni katika kurejesha kwa jamii kile walichompa yeye na hivi karibuni alifanya alambee na kukusanya Mil. 2 katika eneo la Naguru.
Hii inafuatia baada ya wasanii wengine nchini humo Iryn Namubiru na Angella Katatumba walioanzisha taasisi hivi karibuni.
Wasanii wa kibongo mpo hapo!!!

RONALDO ATUA MADRID RASMIIIIII



Hatimaye C.Ronaldo ametua katika klabu ya Real Madrid. Hapa ni alipokuwa akitambulishwa kwenye umati unaokadiriwa kufika 80,000 na kuvunja rekodi iliyokuwa ikishikiliwa na Diego Maradona kwa kukaribishwa na watu 75,000.

Monday, July 6, 2009

PRODYUZA KGT, ALIYETENGENEZA CINDERELAA & NAKSHI MREMBO



Huyu ndiye KGT, Mtayarishaji wa studio ya G Records aliyetengeneza nyimbo za Cinderella na Nakshi Mrembo za Ali Kiba. hapa alikuwa studio akifanya mambo kama alivyokutwa na JOHN JOSEPH HARAMBA wa muzikimnene.

KARIBU KWENYE MUZIKIMNENE.BLOGSPOT.COM



Inakuaje watu wangu, mi naitwa JOHN JOSEPH HARAMBA karibu katika blog yenu, vitu ni vingi vya kufurahisha na kukufundisha, mara nyingi sipendi kukupa mambo ya kukusikitisha. Jina la muzikimnene lisikuchanganye. Hii ni blog ya watu wote wakubwa kwa wadogo. kama utakuwa na chochote cha kunishauri au kuchangia check nami kupitia haramba29@yahoo.co.uk au cell phone # +255 713 393542.

KATUNI YA LEO TANZANIA DAIMA



Hii ni katuni ya leo kwenye gazeti la TANZANIA DAIMA imebuniwa na MUSA NGARANGO JR.

Sunday, July 5, 2009

Fab kutua Barca kwa Euro milioni 46



Kwa taarifa zilizosambaa leo kwenye mitandao barani Ulaya, inadaiwa klabu ya Arsenal watakuwa tayari kumwachia kiongo na naodha wao Cesc Fabregas aweze kwenda Barca ikiwa tu mabingwa hao wa kombe la klabu bingwa Ulaya watatoa dau la Euro milioni 46.